TANGAZA NASI LEO

Tuesday, May 29, 2012

Mwenge wa uhuru waendelea kukimbizwa.. upo Mbinga

Kaimu Katibu Tawala wa wilaya ya Nyasa Bi Happy Msanga (kushoto) akikabidhi Mwenge wa uhuru kwa Kaimu Katibu Tawala wilaya ya Mbinga Bw.Iddi Mponda baada ya kumaliza mbio zake katika wilaya ya Nyasa.Tukio hili limefanyika leo katika kijiji cha Chunya wilaya ya Mbinga

BASATA YAWATAKA WASANII KUONGEZA THAMANI KATIKA KAZI ZAO



Huku kukiwa na juhudi za kutambuliwa na kuthaminiwa kazi za wasanii ndani na nje ya nchi, Baraza la
Sanaa la Taifa (BASATA) limewataka wasanii kuongeza thamani kwenye kazi zao ili
kuzipa ubora zaidi.
Wito huo umetolewa mapema wiki hii na Mkurugenzi wa Idara ya Utafiti, Mafunzo na Habari wa BASATA Godfrey Lebejo wakati akihitimisha programu maalum iliyohusu Ubunifu, Utengenezaji na
Uongezaji thamani katika Kazi za Sanaa kupitia Jukwaa la Sanaa.
Alisema kuwa, ubora katika Sanaa unapatikana pia kwa Wasanii kuangalia wenzao wanafanya nini na wao kupata ubunifu mpya kwa kuongeza vionjo, uthamani na ubunifu binafsi katika kuifanya
kazi ya Sanaa kwanza kupendwa na baadaye kupewa thamani kubwa sokoni.
“Ni wazi Wasanii wetu wanapaswa kuzingatia uongezaji uthamani kwenye kazi wanazozifanya. Kubuni kazi ni suala moja lakini kuongeza uthamani katika kazi yako ili ivutie wengi na
kuuzika kwa thamani kubwa ni suala lingine la kuzingatia” alisistiza Lebejo.
Aliongeza kuwa, kwa sasa kuna taarifa za Wakenya kununua kazi za Wasanii wetu kwa bei ya chini na
baadaye kuziongezea ubunifu, thamani na kuziuza nje kwa bei  kubwa. Katika hili
anasema, inatokana na wasanii wetu kutokuzingatia falsafa hiyo ya ubunifu na uongezaji thamani wa
kazi zao.
“Tuna bahati ya kuwa na malighafi nyingi sana, baadhi zimeoneshwa hapa lakini suala hapa ni sisi
kutumia ipasavyo malighafi hizo katika kubuni kazi zenye ubora na kuhakikisha
tunazipa thamani stahiki tunapozisafirisha nje” alizidi kusisitiza.
Awali akiendesha darasa hilo maalum ambalo wiki hii lilikuwa mahsusi kwa ajili ya wasanii na
wajasiriamali wa Sanaa za mikono (Handcrafts), Haroun Sabili kutoka asasi ya
Musoma Handcraft alisema kuwa, Sanaa hizo zinahitaji ubunifu na umakini mkubwa
kwani kinyume chake ni kutokuvutia na kupoteza uthamani.
Alitoa wito kwa Wasanii kujiunga katika vikundi na kuwa rasmi ili kuhakikisha kwanza,wanajenga
mazingira ya kuwezeshwa lakini pia kupata mafunzo mbalimbali ambayo yatawafanya
wazalishe kazi za Sanaa zenye ubora na thamani kubwa.
“Ni ngumu sana kuhudumia msanii mmoja-mmoja lakini mkiwa kwenye umoja ni rahisi sana kupata fursa za uwezeshaji hususan mafunzo katika kuongeza ubunifu na uthamani wa kazi zenu”
alishauri Haroun.
Katika programu hiyo iliyohudhuriwa na wadau 72, elimu kuhusu ubunifu na uongezaji thamani kwenye
kazi za Sanaa ilitolewa sambamba na malighafi mbalimbali na jinsi zinavyoweza
kutumika kuzalisha kazi za mikono kuoneshwa.

MEDIA BRIEFING NOTE FOR THE GLOBAL 2013 SMART PARTNERSHIP DIALOGUE TO BE HELD IN DAR ES SALAAM, TANZANIA – 24TH TO 28TH MAY, 2013



Tanzania will host the next Smart Partnership Dialogue that is scheduled to take place from 24th to 28th May, 2013 in Dar es Salaam. President Jakaya Mrisho Kikwete, is  expected  to officiate the  National launch at noon  today Tuesday May 29, 2012 at the Karimjee Hall grounds in Dar es salaam.
President Kikwete had agreed to host the event  during the last dialogue that took place in Putrajaya, Malaysia in June, 2011  -  branded the Langkawi International Dialogue.
The Smart Partnership Dialogues are a brainchild of the Commonwealth Partnership for Technology Management. The CPTM which is the social and scientific interlinkage arm of the Commonwealth, has since 1995 undertaken in collaboration with willing national partners to provide a forum that cuts across the east-west, have, have not’s and the developed and developing dichotomy for the discussion of topical subjects in a conducive inclusive, open dialogue. Inspired by the increasing need to ensure a win-win interrelationship between actors, the CPTM, in collaboration with the host country undertake to provide an ambient setting where individuals from all walks of life and professions can meet and hold serious discourse on selected subjects every two years.
To ensure that these dialogues are successful, a two pronged approach is utilized. The first is when the host country convenes a National Dialogue. This involves the gathering together of different sectors of the host community and coming up with a topical issue that is not just locally relevant, but which resonates internationally and merits a grander discourse and focus. The second is when the Host country in collaboration with the CPTM plan for, invite participants and hold an international open dialogue on the selected topic, in essence, host aSMART DIALOGUE.
As hosts, the kicking off of the National Dialogue is very crucial. It is a means for creating National and International awareness of the next host of the Dialogue and avails the opportunity to announce the dialogue venue, topic and dates.
The Launch of the National Campaign for the Dialogue in Tanzania will take place on the 29th May, 2012 at the Karimjee Hall Grounds from 10:00 am to 11:00 am. The Host and Patron Advisor for the 2013 |Smart Partnership Dialogue, H.E. Jakaya Mrisho Kikwete, President of the United Republic of Tanzania will officially launch preparations for the 2013 Dialogue and introduce the Theme for the Dialogue (Leveraging Technology for Africa’s Socio-Economic Transformation) announce the date for the Dialogue (24th to 28th May, 2013) and the venue (Dar es Salaam) issue a holistic invitation to both the citizens of Tanzania as well as the International Community at large, and share his vision for the Dialogue. The Dialogue has been branded the GLOBAL 2013 SMART PARTNERSHIP DIALOGUE in anticipation of interest the chosen theme is likely to raise. Technology is a global phenomenon, a global concern, a global topical issue. It is therefore more than likely that a Dialogue on Technology for development shall merit global attention and have a global audience/participation.
The Execution of the preparation will be undertaken under the guidance of the Chief Secretary who is the Convener of the Dialogue. The Chief Secretary will be supported by a National Steering Committee that comprises of Permanent Secretaries from All Ministries as well as Representatives of Keyline Sectors both on Mainland Tanzania and Zanzibar.
A Focal Point Team from the Ministry of Foreign Affairs will spearhead the logistical and liaising activities necessary for the successful execution of the Dialogue. The Team will over time incorporate Members from different Links
A Resource Group with an Advisory role comprising of key members of the Academia, Business and Corporate Community, Youth, Labour, Culture, Industry and Media has been set up under the leadership of Professor Samuel Wangwe.
Following the National Launch, the next step is scheduled to be contact with different Links within Tanzania who will in turn be linked with counterparts interested in participating in the Dialogue in 2013. A National Dialogue to discuss the theme will follow thereafter.
Other African countries that have hosted the Smart Partnership Dialogues include Botswana, Namibia, Zambia, Zimbabwe, Mozambique, Swaziland, Lesotho and Uganda that has hosted it twice. Other countries include Barbados, and Malaysis that has hosted the dialogue nine times.
 Issued by
THE FOCAL POINT TEAM, GLOBAL 2013 SMART PARTNERSHIP DIALOGUE,  MINISTRY OF FOREIGN AFFAIRS AND INTERNATIONAL COOPERATION

Monday, May 28, 2012

RAULA Filamu itakayokimbiza


 
KUNA filamu inakuja , ambayo kwa kuangalia tu mshikemshike  wake kwenye uchukauji lazima ije kuwakimbiza watu.
Utata mtupu, mazingira matata matupu, uchokara lakini  dhuluma na  makasheshe behind the Scene itakuwa noma. Watu wanazimia Scene kali kwelikweli.
Chuchu akiwa katika jeneza

hapa ndipo scene ilipoanza kuwasha

Hii ikawa taabu kwelikweli. Huyo ni Raula, mtoto halisi wa Chuchu
Naam hiyo itakuwa tamu  manake hata Nyota wa filamu wa kike nchini Chuchu Hansi alijikuta akiangua kilio kizito baada ya kumaliza scene ya kuingizwa kwenye jeneza ambako mtoto wake naye anaigiza na alitoa unyende babu kubwa.
Chuchu aliagiza  kama mnke wa mtu aliyekufa aliyeteswa na kufa kwa mateso.
Kasheshe ikaja pale alipolala kwenye jeneza, baada na watu kuja  kuga mwili wake, ndipo mwanaye kipenzi Faria (anayeigiza kama Raula) alipolia kinoma.
Raula alilia kwa hisia kali huku akiita mama!! Mama!!, na kung’ang’amia jeneza huku akitiririkwa na machozi. Hisia kali zilipenya maskioni mwa mama yake wakati wa Scene na kumfanya kushindwa kutoka kwa kilio na kuishiwa nguvu baada ya kumaliza shooting.
Hii sinema we acha tu,Mwigizaji mwingine wakati akiaga (duhh inayotakiwa kuwa maiti ya Chuchu), akiigiza kulia ghafla aliregea na kudondoka chini,  hali iliyopelekea watu kwenda kumuokota na kumweka vizuri.
Tofauti ilivyokuwa kwa Chuchu, kwani mwanamama huyo alipooza kabisa fahamu na kupata tabu katika upumuaji. Ilimbidi kumchukua na kuandaa chumba maalum kwaajili ya kuweka waliozidiwa,  ili kumrudisha katika hali yake ya kawaida. Ilimchukuwa zaidi ya dakika 45 katika kuzinduka na kuwa katika hali ya kawaida huku maombi makali yakipigwa katika kuhakikisha anarudi kuwa sawa. 
Mauzauza  hayakuishia hapo, hadi kwa mwigizaji maarufu na mkongwe Rachel ambaye alishaigiza filamu nyingi za kulia, lakini hapo alijikuta akizidiwa kiasi cha kulia mpaka kupata maumivu makali ya kichwa.   Naye ilibidi achukuliwa haraka na kupelekwa kwenye chumba maalum kwaajili ya kupata huduma, kwani alikuwa akilalama kwamba hali yake sio nzuri kabisa, kutokana na maumivu ya kichwa.
Kwa habari zaidi nenda http://www.bongounit.blogspot.com

ZANZIBAR HALI SI SHWARI

MADHEBAHU YA KANISA LA T.A.G KARIAKOO ZANZIBAR

UPANDE WA MADIRISHA YA KANISA LA T.A.G KARIAKOO ZANZIBAR

UPANDE WA MADIRISHA YA KANISA LA T.A.G KARIAKOO ZANZIBAR

MABAKI YA VITU VILIVYOTUMIKA KURIPULIA KANISA HILO

MCHUNGAJI DICKSON KAGANGA WA KANISA LA T.A.G KARIAKOO AKIONGEA NA WAANDISHI WA HABARI KANISANI HAPO

WAUMINI WAKIWEKA SAWA MABAKI

MCHUNGAJI DICKSON KAGANGA WA KANISA LA T.A.G KARIAKOO AKIONGEA NA WAANDISHI WA HABARI KANISANI HAPO

UFA ULIOSABABISHWA NA MRIPUKO

WAUMINI WAKIJADILI JAMBO NYUMA YAO KUKIWA NA BAADHI YA MABAKI VIKIWEMO VITI

WAUMINI WAKIZIBA MADIRISHA TAYARI KWA IBADA
GARI ILIYORIPULIWA NDANI YA ENEO LA KANISA LA T.A.G KARIAKOO ZANZIBAR

KANISA LA T.A.G KARIAKOO LIKIWA KATIKA HALI MBAYA

ASKARI WA KUTULIZA GHASIA AKIWA KAZINI MJINI ZANZIBAR

MAENEO YA MICHENZANI MATAIRI YALICHOMWA

ASKARI WA KUTULIZA GHASIA LEO ASUBUHI WAKIHAKIKISHA USALAMA UNAKUEPO

HUO NI MOSHI WA MATAIRI UKIWA UMECHANGANYIKA NA MABOMU YA MACHOZI

HAPO NI HARAKATI ZA KUTULIZA GHASIA

MICHENZANI USIKU WA KUAMKIA LEO

MICHENZANI PAKIFUKA MOSHI

MSHIKE MSHIKE

Beda Msimbe reflections :mwenye akili na asiyekuwa na akili kwa kawaida lao moja


KWA sasa Tanzania imeingia katika wimbi kubwa la kushabikia matatizo yanayoambatana na ufujaji wa fedha, wizi, rushwa na ufisadi; zipo pia kauli mbalimbali zinatolewa kuhusiana na matatizo hayo, chimbuko lake na laana inayoambatana nayo.
Mimi sina shaka na kampeni hii ya kuondoa udhalimu katika maisha ya watu ila nina mashaka na wimbo huu unavyoimbwa, wapo watu wanataka zari na wala si shari  na hili lazima niliseme.
Yapo madai kuwa waandishi wa habari ni kioo cha jamii. Lakini bila kujali uprofesheni au la, waandishi ambao kihistoria wapo tangu enzi za kale katika majina tofauti ni watu hatari sana wanapoamua kufanya mambo kiutata hasa pale wanapoamua kwa makusudi mazim akushabikia au kutoa habari iliyopwelea vitu  kibao.
Bila hata kuuma meno  kwani na mie nimo (inafaa wakati mwingine kumla jongooo kwa kung’ata meno mbichi) tunachekelea hatari kwa kuandika vilivyonusu nusu na kupeleka kwa jamii ambayo  inatarajia tuchambue na tuwape nafasi wao waamue na si kwa kuwapeleka kama maiti kwenda kuzikwa.
Kwa ufupi tunaifanya jamii kuwa yenyewe haina daraja, haijui vibaya na ambayo haiwezi kuchambua mambo wala kujenga msingi mzuri wa kuelewa chimbuko na kutafuta mgogoro wake.
Kama utaangalia sentensi ya kwamba, ukichambua magazeti hata yale uliyosoma wiki hii utatambua kwamba kioo hiki cha jamii kina walakini, kina tope na wote tunaojitazama tunajiona kuwa tuna tope kumbe tupo waa bila doa.
Naam, watu wanadhani ni masikhara lakini kalamu ni silaha mbaya kuliko hata bomu la nyukilia. Bomu likiua kifizikia,kalamu huua kiakili na kumfa nya mtu asiwe kabisa na haja wala nia ya kufanya vitu vyenye maana duniani akibaki kuwa mbeya na shambenga mkubwa.
Mimi ningelipenda kuzungumza sana kuhusu ushambenga na umbeya kwani si ndivyo ilivyo?!
Mathalani miaka ya karibuni Wasauzi walikuwa na jihadi ya aina yake waliwashambulia wageni kwani wamewapoka utajiri wao. Kimsingi mashambulio hayo unaweza kuyaona kama yanatokana na matatizo ya kiuchumi lakini kiutaalamu ni tatizo la kisosho  kwani kimsingi wakishamalizana  na wageni ambao ni waswahili wenzao watawaibukia, wazungu na wahindi na wakishawamaliza wataanza kuwaangalia Wakosa na Wazulu kisha nani ni nani katika makabila ya wenyewe.Itakuja wewe si wa ukoo wangu.Nataka kusema ile ni dhambi ya ubaguzi
Habari ndio hiyo.
Nasema ndio hiyo kwa kuwa matatizo mengi ambayo yamesababishwa na magazeti ambayo yametengeneza kuwa wageni (huko) wanashika nafasi ya kazi na wenyeji wanakosa huku wakisahau kuwa kila Ijumaa wanapokea fedha za kazi na hawarudi kazini mpaka fedha hizo zimeisha Jumanne.
Pia wanasahau kuwa wao wakishapata fedha hawarejei nyumbani kabisa na wala watu wao hawawezi kuwa na akiba ya fedha za maendeleo, watoto hawaendi shule na watanzania waliodhamiria kubadili maisha wanakubali kulala katika maguni na kurejesha fedha nyumbani.
Mimi naamini nikikumbuka, magazeti na vyombo vya habari local vimechangia sana mtafaruku ule, ndio maana nathubutu kuuliza kioo kikiingia uchafu  inakuwaje vile?
Wanawake wa Afrika kusini wapo tayari kubembelezana na wahamiaji kwa kuwa wanajua wanafanya nini, wanataka nini na wanawajali lakini si wanaume wao ambao umkomboti ndio dawa inayotitibua ufanisi katika kazi.Haya si matusi ni mifano halisi tu katika jumuiya.
Naam hao ni waafrika kusini tatizo la kijamii wameligeuza la kiuchumi na kuwaswaga wenzao, dhambi hizo ama hakika zitawarejea hata wao kama mwalimu Nyerere alivyokwishawahi kusema mkishamaliza huko pembeni hakika mtarejea nyumbani mkamalizane.
Dhambi ya kula nyama ya mtu si ya kawaida, kwani lazima itaendelea kutafuna wengine.
Tuache hayo ya mathalani ya Afrika Kusini turejee hapa nyumbani Hivi.Wakati mwingine ni kweli kuwa tunaandika tukitambua kwa kufanya hivi tunahatarisha vitu vingi, lakini tunasukumwa tukiamini kuwa ustawi wa taifa ndio dira kumbe unakula kasumba ambayo ungeliifua zaidi ungelitambua kwamba ni bangi la kukupumbaza.
Wapo watu wanatoa hoja uchwara kuhusu ufisadi, kuhusu rushwa na kuhusu mambo mengi ambayo kimsingi hayana maana kusimuliwa lakini tugeuza gumzo tunaacha kitu cha msingi.Ndio inawezekana kabisa, lakini je umeshajiuliza maswali kadhaa kabla hujatoa konklusheni?
Swali la kwanza nini laifu staili ya mtu?
Swali la pili nini kinamfadhaisha mtu katika maisha yake?
Swali la tatu unajua kwamba si kila mgonjwa hufa mara moja lakini kila mzima hufa dakika ile ile anayotakiwa kufa?.
Nani alisema kwamba  ukiugua huruhusiwi kufa na pia ukiwa mtu mzima huruhusiwi kufa?
Je kama ni kweli kuwa kufa lazima kuwe na sababu na anayeliwa na simba ni nani kachonga mingo ya mauaji?
Ningelipenda usinielewe kabisa, kwani ukinielewa hutaleta shida.Waandishi wa habari tunaweza kuleta  shida sana katika maisha kama kila kitu tutakichukua kama kilivyo halafu mseme kwamba kuna mkono wa mtu. Nina shaka kubwa huu mkono wa mtu si wa kweli.
Huenda hali ya mashaka inatokana na waandishi wa habari kuchukua sana maneno ya mitaani, kutochambua inavyostahili na kushikilia maelekezo mzunguko yanayofanywa na maspinidokta ili mradi waue sooo wanayotaka kwa kupakazia upande mwingine, wataalamu wa lugha za kifisadi wanasema ni blackmail.
Halafu si unajua tena kuna matangazo mengi, haya magazeti ya kwenye mitandao ambayo inawafanya watu kitu mbaya kabisa.Inachukua tu yenyewe si watu wanaposti, lakini mimi najua si bure kila kitu kilichoingia kitakuwa kimetiwa baraka na mhariri wa tango hilo au la basi ni gumzo ambalo ingawa si makini ni kichocheo cha fikira na watu wakilimeza bila taarifa mambo huenda kuwa kama mlevi wa gongo.Na wapo watu wanaoamua kuwalewesha watu wengine.
Unapokuwa na watu wa aina hii ambao ndio mhimili wa taarifa za dunia basi ujuwe walakini mkubwa upo labda kukosekana kwa namna bora ya kuwasilisha hoja kwa kufuata mikondo inayoeleweka.
Unapokuwa na chuki binafsi masuala ya kizandiki lazima yajichanue lakini unapokuwa humpendi fulani upuuzi wa kutunga uzushi lazima utakuwepo na unapoona kuna kitundu tu kidogo unautangaza uwongo huo ambao unakuwa mkubwa na unaokubalika kuliko shauri la majimaji alilolianzisha kinjeketile kwa ajili ya kuwakomboa watu wake kutoka utumwani.
Rais Jakaya Kikwete wakati wa tuzo za uandishi mahiri,EJAAT, hili nisiliseme aliasa waandishi wa habari waachane na uongo waandike ukweli, waachane na chuki za kisasiasa wahabarishe wao ndio nguzo ya jamii,sasa mimi nasema na tufanye utafiti wa kina kabla ya kukubali tuhuma zozote zile tunazoambiwa:kwani inawezekana kabisa tupo ambao lazima tufe kwa staili yetu ya maisha na pia lazima tufe kwa sababu tunadhani muda bado.
Nataka kusema tchao kwani mwenye akili na asiyekuwa na akili kwa kawaida lao moja wanapishana digrii ya utekelezaji.